SERIKALI YAMPONGEZA DIAMOND KUCHAGULIWA BET

MKURUGENZI wa Idara ya Habari
Maelezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amempongeza
msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz kwa kuchaguliwa
kuwania tuzo za BET mwaka huu 2021.
Akiwa ndiye msanii pekee kutoka
Afrika Mashariki aliyechaguliwa kuwania tuzo hizo, Diamond amechaguliwa kuwania Tuzo katika kipengele cha 'Best
International Act' akiwa pamoja na Mastaa kama Wizkid, Ayana
Kamura, Burna Boy, Young Tand.
"Kongole @diamondplatnumz Hujawahi kutuangusha." aliandika Msigwa
kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Post a Comment