SERIKALI YAMPONGEZA DIAMOND KUCHAGULIWA BET

 

LIVE SIMU YA GERSON MSIGWA KWENYE KIPINDI CHA BARAGUMU LIVE - YouTube

MKURUGENZI wa Idara ya Habari Maelezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amempongeza msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz kwa kuchaguliwa kuwania tuzo za BET mwaka huu 2021.

Akiwa ndiye msanii pekee kutoka Afrika Mashariki aliyechaguliwa kuwania tuzo hizo, Diamond amechaguliwa kuwania Tuzo katika kipengele cha 'Best International Act' akiwa pamoja na Mastaa kama Wizkid, Ayana Kamura, Burna Boy, Young Tand.


"Kongole 
@diamondplatnumz Hujawahi kutuangusha." aliandika Msigwa kupitia ukurasa wake wa Instagram.

 

No comments