QUEEN SENDIGA MPINZANI WA KWANZA SERIKALINI


Sendiga.jpg


 SIKU chache baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kutoa kauli kuwa atafanya kazi na mtu yeyote bila kujali itikadi yake ya kisiasa, leo ameiishi baada ya kumteua Mgombea Urais wa Chama Cha Upinzani cha Alliance For Democratic Change (ADC), katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, Queen Sendiga kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa.

Queen Sendiga anachukua nafasi ya Mkuu wa Mkoa huo, Ali Hapi ambaye amehamishiwa mkoa wa Tabora.

Wakati wa utawala wa serikali ya awamu ya tano chini ya hayati John Pombe Joseph Magufuli, viongozi wawili waliingizwa katika utumishi serikalini wakiwa bado viongozi wa vyama vya upinzani.

Hao ni aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira ambaye wakati huo alikuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha ACT na aliyekuwa kiongozi mwingine wa chama hicho, Dk. Kitila Mkumbo ambaye aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji.

Wakati wa kampeni zake za kuutafuta urais wa Tanzania, Queen alikuwa akipiga kampeni zake kwa kuwafuata akina mama kwenye shughuli zao, akienda sokoni, stendi za mabasi na hata katika mihangaiko mingine ya wanawake.

Aidha, wakati wa kampeni hizo, alikuwa akimuunga mkono aliyekuwa mgombea urais wa CCM, Hayati John Magufuli na mara kadhaa, alisikika akimuomba Rais Magufuli amkumbuke katika utawala wake.

 

 

No comments