OMBAOMBA WA WHEEL CHAIR WATOWEKA DAR


China Topmedi Smart foldable Power Electric Wheel kwa Walemavu, jumla ya  Kiti cha Magurudumu kwenye TopChinaSupplier.com

WAKATI agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makala la kutaka watu wote wanaojihusisha na ombaomba kuondolewa, imebainika kuwa wale ombaomba waliokuwa wakitembezwa kwenye viti maalum vya wasiojiweza (Wheel chair) hawapo tena mitaani.

Habari ambazo bado Ojuku blog haijazithibitisha zinadai, wananchi hao walikuwa ni mradi wa mtu, aliyewakusanya kutoka mikoani na kuwajaza katika nyumba yake, akiwapatia mahitaji muhimu, kisha akiajiri watu wa kuwatembeza ambao walikuwa wakimletea hesabu.

Vyanzo vinasema mtu huyo amekamatwa na uchunguzi unaendelea.

No comments