MTAKA AWALIPUA VIONGOZI WAJINGA WANAOBEZA SEKTA BINAFSI


Hon Anthony Mtaka on Simiyu Region Investment Guide Video - YouTube

WAKATI viongozi wengi wa serikali walioteuliwa au kuchaguliwa na wananchi wamekuwa kama vile hawaoni mchango wa sekta binafsi katika maendeleo ya nchi, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amewalipua viongozi wa namna hiyo na kuwaita WAJINGA.

Akizungumza wakati wa kikao cha kuwekeana mkakati mkoani Dodoma, RC Mtaka amesisitiza uongozi unapatikana kwa kuchaguliwa kwa kura au kuteuliwa, Lakini kuna wakati wananchi wanaweza kumpigia kura mtu mjinga na akawa kiongozi wao na kujiona Serikali ni kila kitu lakini sio sekta binafsi.

Hata hivyo anasema yawezekana mtu akateuliwa pia akawa mjinga na kuanza kudharau sekta binafsi, Anasema kwake sekta binafsi ni ufunguo wa maendeleo, hivyo amewaomba watumishi kuheshimu sekta binafsi.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma RC Mtaka anasema viongozi wa Serikali waheshimu sekta binafsi kwani kufanya kazi binafsi kunahitajika akili kubwa, Viongozi wengi wa Serikali hawawezi hata kujiajiri ingawa wanalipwa mshahara wengine mpaka milioni mbili, mpaka wakistaafu ndio wanaheshimu sekta binafsi.


 

No comments