LAMINE MORO ATIMULIWA KIKOSINI YANGA

 Yanga SC defend move to hand defender Moro captaincy armband | Goal.com

NAHODHA wa mabingwa wa kihistoria nchini, Yanga, Lamine Moro ametimuliwa kambini baada ya kutokea kwa sintofahamu baina yake na Kocha Nasraddine Mohammed Nabi.

Yanga ambayo ipo Ruangwa mkoani Lindi kujiandaa kwa mechi ya baadaye jioni ya leo dhidi ya wenyeji Namungo, imemuamuru beki huyo kisiki raia wa Ghana, kurejea jijini Dar es Salaam.

Msemaji wa klabu hiyo, Hassan Bumbuli amenukuliwa akisema Lamine ameamriwa kurejea Dar na kocha baada ya kutokea sintofahamu baina yao jambo ambalo halikuwa na afya kikosini.

 


No comments