HOYCE TEMU ANASTAHILI UBALOZI

KUFUATIA uteuzi uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan jana wa mabalozi na kutajwa kwa jina la Hoyce Temu, wengi wamejawa na mashaka na kujiuliza ni kwa jinsi gani mrembo huyo aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 1999 anaiweza nafasi hiyo.
Ukweli ni kwamba Hoyce,
ambaye alijipambanua kama Miss Tanzania pekee kujikita katika shughuli za
kijamii hata baada ya kuvua taji hilo, anastahili nafasi hiyo kwani licha ya
sifa nyinginezo, alisoma Stashahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Mahusiano ya
Kigeni yaani Post Graduate Diploma in Management of Foreign Relations (PGD-MFR)
kutoka Chuo cha Diplomasia Kurasini Dar es Salaam na Mozambique-Tanzania Centre
for Foreign Relations (CFR).
Hoyce Temu aliwahi kuhudumu Umoja wa Mataifa Tanzania (UN-Tanzania) kama Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano lakini pia alipata kuhudumu kama Mtaalamu wa
Mawasiliano UN-Tanzania (UN Communication Specialist) na pia Mchambuzi wa Mawasiliano
au UN Communication Specialist.
Hivyo Hoyce Temu ana taaluma ya Uhusiano wa Kimataifa na Diplomasia kutoka Chuo
cha Diplomasia na zaidi ya hilo ana weledi wa masauala ya kidiplomasia kutokana
na kufanya kazi UN ofisi ya Tanzania.
kwa kifupi, alichosoma Hoyce Temu ndicho walichosoma maafisa wa Wizara ya Mambo
ya Nje ambao kikanuni ni lazima wasome kozi za Chuo cha Diplomasia (CFR) kama
kigezo kimojawapo cha kutoka ngazi moja ya daraja kwenda lingine ili waweze
kumudu majukumu yao ipasavyo.
Credit: Jamii Forum

Post a Comment