AKINA MDEE WANAWEZA SAMEHEWA CHADEMA

HUKU wanachama na mashabiki wa chama kikuu cha upinzani nchini, Chadema wakitaka wanachama 19 waliovuliwa uanachama kwa kosa la kujitangaza ubunge wa viti maalum na kuapishwa wafukuzwe, kuna dalili kuwa wabunge hao wanaweza kusamehewa.
Dalili hizo zinakuja kufuatia kauli ya Mwenyekiti
wa Taifa wa chama hicho Freeman Mbowe aliyoitoa jana akiwa katika kikao cha
ndani mjini Bunda mkoani Mara.
Mbowe alikaririwa akisema endapo wanachama hao 19
waliofukuzwa wakirudi na Baraza Kuu likawasamehe hakuna shida yoyote, anawafahamu
vizuri kwani wamekuwa watu wake wa karibu zaidi ya wanachama wanavyofahamu.

Post a Comment