Zlatan: Sijamuona Ronaldo Italia, Ronaldo ni mmoja tu, yule Mbrazil

Pichani kulia, Zlatan akisalimiana na Ronaldo Mreno wakiwa na timu zao za Taifa na kushoto, Msweden huyo akimkabidhi jezi legendari wa Brazil, Ronaldo de Lima

 

Mtandao wa AiScore Sports, unaojihusisha na habari za michezo na wanamichezo, umeripoti leo kuwa mshambuliaji wa Sweden na AC Milan, Zlatan Ibrahimovic amemponda nyota wa Juventus, Christiano Ronaldo, raia wa Ureno.

"Unaniuliza kama nimemuona Ronaldo halisi Italia? Sijamuona, kuna Ronaldo mmoja tu, yule Mbrazil."

"Cristiano Ronaldo alijisajili timu ambayo imeshinda taji la Serie A mara saba mfululizo. Kwenda katika klabu kama hiyo hupati changamoto. Kama ninataka changamoto kweli, ningeenda Juventus ikiwa Serie B nipambane kuipandisha na kuiweka juu."

 


 

No comments