Adriano auza nyumba, ahamia hotelini
Adriano Leite Ribeiro, maarufu kama Adriano, nyota wa zamani wa Brazil, haishi vituko. This time, mshambuliaji huyo wa zamani wa Parma na Inter Milan za Italia, ameuza nyumba yake yenye thamani ya paundi milioni 1.2 sawa na shilingi za kitanzania 348000000 (3.48bilioni).
Nyumba hiyo ipo
eneo liitwalo Barra da Tijuca, linalokaliwa na watu wa daraja la juu magharibi
ya jiji la Rio de Janeiro nchini Brazil.
Lakini baada ya
kuiuza nyumba hiyo hiyo, aliacha kila kitu kilichomo ndani yake, isipokuwa medali
zake tu alizotwaa enzi akicheza soka na kwenda kupanga chumba hotelini ambako
analipa dola 10 (sawa na shilingi za kitanzania 23,000) kwa siku.
Adriano, ambaye
wakati akiibuka katika soka miaka ya mwanzoni mwa 2000, akitajwa kama mrithi wa
Ronaldo de Lima, alishindwa kufikia matarajio baada ya kuanza maisha ya starehe
na unywaji pombe uliopitiliza.

Post a Comment