WATU WAKANYAGANA KUMUAGA MAGUFULI


Ni full. Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam wenye uwezo wa kuingiza watu 40,000 waliokaa, leo umejikuta ukizidiwa, baada ya watu wengi kuliko maelezo kuingia katika harakati za kumuaga Mwamba, Dokta John Pombe Joseph Magufuli.

JPM aliyefariki Machi 17 mwaka huu, anaagwa kwa mara ya mwisho na wakazi wa Dar es Salaam leo kabla ya jioni kupelekwa Dodoma ambako wakazi wake watapata fursa hiyo kesho, itakayofanyika katika Uwanja wa Jamhuri.

Ratiba pia inaonyesha wananchi za Zanzibar na Mwanza nao watapata fursa ya kuaga kabla ya mwili wake kulazwa katika nyumba yake ya milele, kijijini kwao Chato Mkoani Geita Ijumaa hii.

No comments