Samia kuapishwa leo, JPM kuzikwa Chato
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ataapishwa leo asubuhi hii saa nne, Ikulu jijini Dar es Salaam kuwa Rais wa Sita wa Tanzania.
Mama Samia anachukua nafasi ya Rais
John Magufuli, aliyetangazwa kufariki Jumatano Usiku Machi 17, 2021.
Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt
Hassan Abbas, aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa mwili wa JPM utaagwa
katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Mwanza, kabla ya kufikishwa Chato kwa
mazishi.

Post a Comment