Raila atoka Hospitalini
KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga
ameruhusiwa kutoka hospitalini alikokuwa amelazwa baada ya kupatwa na virusi
vya korona, Covid 19.
Raila, Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya mwenye
umri wa miaka 76, alilazwa tangu Machi 9 mwaka huu, baada ya daktari wake
kusema alikuwa akijisikia maumivu ya mwili na uchovu.
Ikiwa ni mwaka
mmoja toka Kenya ipate mgonjwa wa kwanza, nchi hiyo imerekodi watu 110,000 kuugua ugonjwa huo, 87,903 wakiripotiwa
kupona na vifo zaidi ya watu 2,000.
Mwanzoni mwa
ugonjwa huo, Utawala wa Rais Uhuru Kenyatta ulipiga marufuku mikusanyiko ya
kisiasa, kufunga sehemu kubwa ya shughuli za kijamii na kiuchumi.

Post a Comment