Diamond ampaisha Haji Manara

 

Diamond Platnum, msanii maarufu zaidi wa Tanzania, ambaye pia ni CEO wa Wasafi Media, jana usiku alimtembelea Msemaji wa Simba Haji Manara, nyumbani kwake, Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Diamond aliyeongozana na msanii aliye chini ya lebo yake ya WCB, Mbosso pamoja na baadhi ya staff wake wa Wasafi, alishiriki pia chakula cha usiku, kilichoandaliwa na mke wa Manara, Naheeda Abdallah.

Hii inakuja siku chache baada ya msemaji huyo kuwa katika mzozo mkubwa uliomalizwa kiutu uzima na mtangazaji wa Wasafi FM, Maulid Kitenge.

Diamond ambaye jina lake lingine la utani ni Simba, ni shabiki kindakindaki wa klabu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi

No comments