Huyu ndiye John Joseph Pombe Magufuli
·
1959- Azaliwa Chato kaskazini
magharibi mwa Tanzania
·
1995- Achaguliwa kuwa mbunge kwa
mara ya kwanza
·
2000- Ateuliwa kuwa Waziri
·
2015- Achaguliwa kuwa rais kwa
muhula wake wa kwanza
·
2020- Achaguliwa kwa kipindi cha
pili kuwa rais
·
2020 Novemba tarehe 5 – Aapishwa
kwa muhula wa Pili
·
2021 Machi Tarehe 7- Uvumi
unaanza kuenea kuhusu aliko rais Magufuli baada ya kukosa kuonekana kwa muda wa
wiki moja
·
2021 Machi tarehe 11 – Vyama
mbali mbali vya Upinzani nchini Tanzania vyataka kujua hali ya rais Magufuli na
aliko
·
2021 Machi Tarehe 12 -Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa akana kwamba rais Magufuli anaugua asema yupo ‘ buheri wa
afya na anaendelea kuchapa kazi’
·
2021 Machi Tarehe 15 – Makamu wa
Rais Samia Suluhu awapa Watanzania ‘salamu’ kutoka kwa Rais Magufuli huku hofu
ikizidi kuhusu hali yake na aliko
·
2021 Machi, tarehe 6 – Alazwa
katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete kwa tatizo la moyo la mfumo wa umeme
·
2021 Machi tarehe 7 –
Aliruhusiwa kurejea kazini
·
2021 Machi tarehe 14 –
Alikimbizwa Hospitali ya Mzena Dar es Salaam kuendelea na matibabu
·
2021 Machi tarehe 17 saa kumi na
mbili jioni – Magufuli afariki dunia
·
2021 Machi tarehe 17 Usiku –
Makamu wa rais Samia Suluhu atangaza kupitia runinga kifo cha rais Magufuli
.Siku 14 za maombolezo zatangazwa.Bendera kupeperushwa nusu mlingoti.

Post a Comment