Salaam za rambirambi zamiminika Tanzania
Kufuatia kifo cha
Rais John Pombe Magufuli kilichotangazwa jana Machi 17, 2021, salam za
rambirambi zimetumwa kutoka kwa viongozi na wasanii mbalimbali duniani.
Waziri Mkuu wa
Uingereza Boris Johnson aliandika katika ukurasa wake wa Twitter, akielezea
masikitiko yake kufuatia kifo cha Rais Magufuli.
Rais
wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi ametoa salamu za pole kwa
taifa la Tanzania kufuatia kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. John Magufuli.
Rais
wa Somalia Mohamed Farmaajo ametoa salamu za pole kwa Tanzania kufuatia kifo
cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli.
Kwa
niaba yangu na kwa niaba ya Serikali na taifa la Somalia, ningependa kuwasilisha
rambi rambi zetu kwa Jamhuri ya Muungano wa #Tanzania kwa kumpoteza Kiongozi Rais John
Magufuli. Tunalitakia taifa Zima na Serikali subra na utulivu katika kipindi
hiki cha maombi na maombolezo. pic.twitter.com/cQz3rALaPt
— Mohamed Farmaajo (@M_Farmaajo) March 17, 2021
Rais
wa Venezuela Nicolás Maduro ametoa salamu za pole kwa Tanzania kufuatia kifo
cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli.
Waziri
wa Mambo ya Nje wa Kosovo Behgjet Pacolli ametoa salamu kwa Tanzania kufuatia
kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan ametangaza
kifo cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli
aliyefariki dunia Machi 17, 2021 majira ya saa 12:00 Jioni.
Mama Samia amesema Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli amefariki kwa maradhi ya moyo katika hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Licha ya viongozi hao wa kisiasa, pia wasanii mbalimbali, wakiongozwa na Bob Wine wa Uganda, nao walituma salamu zao za pole kufuatia msiba huo mkubwa. Nyota wa muziki wa Uganda pia, Jose Chamilion naye alituma salamu za pole kwa watanzania kwa msiba huo mzito.
Nyota namba moja wa Bongo Flava nchini,
Diamond Platnumz alituma salam za pole kwa familia, Makamu wa Rais na watanzania
wote juu ya msiba huo, kama alivyofanya Vanesa Mdee, Shilole na wengineo
kadhaa.
Related ArticlesLiLi

Post a Comment