David Beckham : Kipaji kinamponza Messi
"Kama umejaribu kugundua kitu
kwa miaka mingi sasa, popote ambapo Barcelona watapoteza mchezo, vyombo vyote
vya habari huonyesha/hutumia picha za
Lionel Messi, kiasi kwamba kila mmoja anaweza kupeleka lawama za kufungwa
kwake.
Lakini Juventus au klabu zingine
zikifungwa, haraka utaonyeshwa picha ya Pirlo na makocha wengine na siyo
mchezaji mmoja, kwa mfano wakati Tottenham ikifungwa, watamuonyesha Jose
Mourinho.
Sitaki kusema kuwa hii ni ajenda ya
vyombo vya habari dhidi ya Messi, lakini iko wazi kwa mtu anayefikiri. Sipendezwi
na hii tabia, lakini kipaji chake ndicho kinachomponza, haitaji promosheni au
kukuzwa na watu wa masoko.
Hii ndiyo sababu siwezi kukataa
kabisa juu ya nafasi yangu ya kumsajili katika klabu yangu ya Club Inter Miami,
Ni mtu mwenye changamoto nyingi, lakini kipaji chake kinafunika mambo yake
yote."

Post a Comment