Dar kumuaga Magufuli kwa siku mbili
Mkuu wa Mkoa wa Dar es
salaam Aboubakar Kunenge ametoa ratiba na utaratibu wa kutoa heshima za mwisho
kwa mwili wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Marehemu Dkt.
John Magufuli ambapo Mkoa wa Dar es salaam umepewa siku mbili za kutoa heshima
za mwisho.
Akitoa ratiba hiyo RC Kunenge amesema kesho Jumamosi March 20
kuanzia saa 1:00 -3:00 asubuhi itafanyika Misa takatifu Kanisa Katoliki Mt.
Petro, saa 3:00 - 3:30 asubuhi, mwili wa Marehemu utawasili Uwanja wa Uhuru,
saa 3:30 - 4:30 asubuhi itafanyika Misa takatifu ambapo saa 4:30 asubuhi hadi
saa 9: 30 alasiri Viongozi wa Serikali, Vyama vya siasa, Wafanyakazi na Taasisi
za Umma watatoa heshima za mwisho na saa 9:30 - 12:00 Wananchi watatoa heshima
za mwisho.
Kunenge amesema Jumapili saa 2:00 asubuhi mwili wa Marehemu
utawasili Uwanja wa Uhuru, saa 2:30 asubuhi hadi saa 10:30 jioni Wananchi
watatoa heshima za mwisho ambapo saa 10:30 Jioni hadi saa 11:00 jioni mwili
utapelekwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambapo saa 11:00 jioni
hadi Saa 11:45 jioni Mwili utasaririshwa kutoka Dar es salaam kuelekea Dodoma.

Post a Comment