Barbara Vs Bestine vita ya pisi kali soka la vigogo

Bestine
WAKATI Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam iliyo katika
hatua za makundi Ligi ya Mabingwa barani Afrika msimu huu, ikiwa na CEO
mwanadada Barbara Gonzalez, As Vita wao wanao Rais wao, mwanamama Bestine
Kazadi ambayo pia inashiriki ligi hiyo hiyo ikiwa kundi moja na Mnyama.
Wakina mama hao wakiwa wanaziongoza timu kubwa barani Afrika,
zinazowania kucheza robo fainali, wanaonekana kama pia kuwa ni wenye ligi yao
nje ya viwanja vya soka, kwani wote wanaonekana warembo, wenye kujua majukumu
yao kikazi.
Barbara, mwanamke wa kwanza kuongoza klabu kubwa ya soka
nchini Tanzania, tokea ateuliwe kuwa CEO wa klabu hiyo, ameonekana kila ilipo
timu hiyo, iwe mikoani katika Ligi Kuu Tanzania Bara, au nje kwenye michuano ya
kimataifa.
Amesafiri pia mara kadhaa kutembelea klabu kubwa barani
Afrika, akiwa na baadhi ya viongozi wa klabu hiyo katika kujifunza jinsi soka
la kimataifa linavyofanywa.
Bestine Kazadi ambaye timu yake kesho inaingia dimbani jijini
Kinshasa kuikabili Al Ahly katika mechi ambayo ni lazima washinde ili waweze
kusonga mbele, amewaahidi wachezaji wake kiasi kikubwa cha fedha endapo
watafanikiwa kuwagonga wababe hao wa soka la Afrika.
Bestine, aliiongoza As Vita kupata sare ngumu ugenini ya
mabao 2-2 dhidi ya mabingwa hao wa kihistoria jijini Cairo, hali iliyowaweka
katika nafasi isiyo na uhakika, ya pili wakiwa na pointi nne, tatu nyuma ya
vinara Simba, walio chini ya Barbara Gonzalez.
Ni nani kati ya wadada hawa atacheka baada ya dakika tisini
kesho? Ni jambo la kusubiri na kuona


Post a Comment