Rais Samia aagiza sekta ya nishati isimamiwe vizuri

 


Rais Samia Suluhu Hassan amesema sekta ya Nishati ina uhusiano wa moja kwa moja wa kiuchumi na kimaendeleo ya maisha ya kila siku ya mwanadamu.

Amewataka wanaosimamia sekta hiyo kutimiza wajibu wao kwa uzalendo mkubwa na kwa kuzingatia kanuni zote za utunzaji mitambo na miundombinu inayotoa nishati ili iweze kupatikana kwa muda wote.

Rais alitoa maagizo hayo kwa Wizara ya Nishati, Shirika la Umeme nchini (Tanesco) na wakala wa umeme vijijini (REA) wakati wa hafla ya kumuapisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt James Peter Matarajio, katika Ikulu ndogo Tunguu.




No comments