Marekani kuanzisha bandari ya muda kwenye pwani ya Gaza kwa ajili ya utoaji wa misaada

 


Rais Joe Biden anatarajiwa kutangaza kwamba jeshi la Marekani litajenga bandari huko Gaza ili kupata misaada zaidi ya kibinadamu katika eneo hilo kwa njia ya bahari, maafisa wakuu wa Marekani wanasema.

Bandari hiyo ya muda itaongeza kiwango cha usaidizi wa kibinadamu kwa Wapalestina kwa "mamia ya mizigo ya ziada" kwa siku, maafisa wanasema.

Hatahivyo, haitajumuisha wanajeshi wa Amerika ardhini huko Gaza, walisema.

Umoja wa Mataifa unaonya kuwa robo ya watu wanakabiliwa na njaa.

Bandari hiyo itachukua "wiki kadhaa" kuanzishwa, maafisa walisema, na itaweza kupokea meli kubwa zinazobeba chakula, dawa za maji, na makazi ya muda. Usafirishaji wa awali utawasili kupitia Cyprus, ambapo ukaguzi wa usalama wa Israeli utafanyika.

Bw.Biden anatarajiwa kutoa tangazo hilo wakati wa hotuba yake hapo baadaye.

Jeshi la Israel lilianzisha kampeni ya anga na ardhini huko Gaza baada ya mashambulizi ya Hamas dhidi ya Israel tarehe 7 Oktoba, ambapo takriban watu 1,200 waliuawa na wengine 253 walichukuliwa mateka.

Zaidi ya watu 30,800 wameuawa huko Gaza tangu wakati huo, wizara ya afya ya eneo hilo inayoendeshwa na Hamas inasema.

No comments