India yabaini mtandao unaoshawishi vijana kwenda vitani Urusi kwa kisingizio cha kazi
Shirika la uchunguzi la India linasema kuwa limebaini mtandao wa maajenti wanaowatuma watu kwenda Urusi nchi yenye vita kwa kisingizio cha kuwapa kazi.
Mawakala hao walikuwa wakiwashawishi watu kupitia mitandao ya kijamii, Ofisi Kuu ya Upelelezi imesema.
Mtandao huo unaenea katika majimbo kadhaa na takriban watu 35 wamekuwa waathirika katika ulaghai huo, shirika hilo lilisema.
Haya yanajiri baada ya Wahindi wawili, ambao walidanganywa kusafiri kwenda Urusi, kuuawa katika vita hivyo.
CBI ilisema katika taarifa kwamba wasafirishaji hao walikuwa wakifanya kazi chini ya "mtandao uliopagwa vizuri".
Ilisema kuwa maajenti walikuwa wakitumia chaneli za mitandao ya kijamii kama vile YouTube na anwani zao za ndani yan chi kuwarubuni vijana kwa njia ya "udanganyifu" ili kuwasafiri hadi Urusi kwa kuwaahidi "kazi nzuri".

Post a Comment