DKT. BITEKO: RAIS SAMIA AENDELEA KUENZI MAONO YA HAYATI MAGUFULI KWA VITENDO
Maono ya aliyekuwa
Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika utekelezaji wa
miradi mikubwa ya Kitaifa kama Ujenzi wa Bwawa la Nyerere, Ujenzi wa Reli ya Kisasa
(SGR), Ujenzi wa barabara na madaraja makubwa kama vile Daraja la Kigongo -
Busisi yametekelezwa na yanaendelea kutekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita
inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Hayo yameelezwa Naibu
Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko katika Misa Takatifu ya kumuombea
Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, iliyofanyika katika
Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yohana Maria Muzeyi Wilayani Chato Mkoani
Geita.
“Niwahakikishie
Watanzaniza kuwa miradi yote ambayo Hayati Dkt. Magufuli akiwa Rais wa Nchi
yetu, Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inaiendeleza yote kwa kasi kubwa ili
tumuenzi kwa vitendo”, amesema Dkt. Biteko.
Dkt. Biteko ameeleza
kuwa Watanzania watamkumbuka Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kwa uwezo wake wa
kiuongozi, karama yake ya kutatua changamoto za wananchi pamoja na
kuwasikiliza, kuondoa kero mahali penye kero, kuhimiza uwajibikaji Serikalini
kwa kuondoa uzembe, ubadhirifu na rushwa.
Misa ya Kumbukizi ya
Miaka Mitatu tangu alipofariki Hayati Dkt. John Pombe Magufuli imeongozwa na
Makamu Askofu, Padri Ovan Mwenge na kuhudhuriwa na viongozi wa Serikali, Chama
cha Mapinduzi (CCM), ndugu, jamaa na marafiki.
Imetolewa na Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi

Post a Comment