Vikwazo vipya dhidi ya Urusi kutangazwa siku ya Ijumaa kuhusiana na vita na kifo cha Navalny

 


Marekani inapanga kuweka vikwazo kwa zaidi ya mashirika 500 na watu binafsi waliohusika katika vita vya Urusi dhidi ya Ukraine.

Vikwazo hivyo, ambavyo vitawekwa siku ya Ijumaa, vitaikumba "Urusi, washirika wake na chombo chake cha vita," Idara ya Hazina ya Marekani ilisema.

Vikwazo vitawekwa na Hazina na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani. Kulingana na Wizara ya Fedha, vitakuwa vikwazo vilkubwa zaidi tangu kuanza kwa uvamizi wa Putin nchini Ukraine.

"Baada ya Urusi kuanzisha vita kamili dhidi ya Ukraine mnamo Februari 2022, Washington na washirika wake waliweka vikwazo kadhaa vinavyolenga mapato ya Moscow , jeshi na viwanda.

Hatua hizi ni pamoja na ukomo wa bei ulioanzishwa na Marekani na washirika wake, unaolenga kupunguza mapato ya Moscow kutokana na mauzo ya nje ya mafuta na bidhaa za petroli.

Wakati huo huo, wakosoaji wanaona kuwa licha ya idadi na sauti kubwa ya vikwazo vilivyowekwa, bado hawajaweza kufikia malengo yao: uchumi wa Urusi sio tu haujapata mkataba tangu mwanzo wa vita, lakini umeendelea kukua ingawa kwa kasi ndogo), na bajeti imepokea mamia ya mabilioni ya dola kutokana na kupanda kwa bei ya nishati.

No comments