Urusi yawachanganya Biden na Trump kuhusu NATO

 


Rais Joe Biden ameutaja ukosoaji wa NATO na mpinzani wake wa uchaguzi wa 2024, Donald Trump, kama usio na maana wa "aibu" na "kinyume na usio wa Kimarekani’’.

Bw Biden alimkemea Bw Trump kwa kusema "ataihimiza" Urusi kumshambulia mwanachama yeyote wa Nato ambaye hafikii kiwango chake cha matumizi ya ulinzi.

Rais huyo wa Marekani alisema matamshi hayo yanasisitiza udharura wa kupitisha kiwango cha msaada wa kigeni cha $95bn (£75bn) kwa washirika wa Marekani.

Mswada huo ndio umepitishwa na Seneti, lakini unakabiliwa na upinzani wa kisiasa katika Bunge hilo.

Katika Ikulu ya Marekani Jumanne, Bw Biden alisema kushindwa kupitishwa kwa kiasi hicho cha pesa - ambacho kinajumuisha $60bn kwa Ukraine - "kutakuwa ni sawa na kuchezea mikononi mwa Putin".

Alisema hatari hiyo imeongezeka kwa sababu ya matamshi "hatari" ya Bw Trump mwishoni mwa juma.

"Hakuna rais mwingine katika historia ambaye amewahi kumsujudia dikteta wa Urusi," Bw Biden alisema.

"Hebu niseme hili kwa uwazi niwezavyo. Siwezi kamwe. Kwa ajili ya Mungu. Ni aibu. Ni hatari. Sio umarekani."

Katika mkutano wa Jumamosi huko South Carolina, Bw Trump, ambaye ni mwanachama wa Republican, alikosoa alichokiita malipo ya "ukaidi" ya wanachama wa Nato.

Trump alielezea kuhusu mazungumzo ya siku za nyuma ambayo alisema alikuwa nayo na mkuu wa "nchi kubwa" kuhusu mashambulizi yanayoweza kufanywa na Urusi.

Bw Trump alisema afisa huyo aliuliza ikiwa Marekani ingemtetea mwanachama wa Nato ambaye hajatimiza wajibu wake wa kifedha.

"Nilisema: 'Hukulipa? Wewe ni mhalifu?'" Bw Trump aliuambia umati. "'Hapana nisingekulinda, kwa kweli ningewahimiza kufanya chochote wanachotaka. Lazima ulipe."

Bw Biden alisema mtangulizi wake alikuwa akiuchukulia muungano wa kijeshi kama njama ya ulinzi.

No comments