Rwanda yasitisha kwa muda mkataba wa mchezaji wa DRC baada ya kuonyesha ishara ya kisiasa uwanjani

 


Chama cha Soka cha Rwanda kimemsimamisha kwa muda kucheza soka nchini humo mchezaji wa kimataifa wa Congo Héritier Luvumbu kwa kuonyesha ishara ya kisiasa wakati wa mashindano .

Mchezaji huyo raia wa Congo anayechezea klabu ya Rayon Sport ya Rwanda anadaiwa kuonyesha ishara hiyo wakati timu yake ilipokuwa ikicheza dhidi ya timu ya polisi ya Rwanda- Polisi Football Club, Jumapili iliyopita wakati wa Ligi Kuu ya Rwanda.

Inasemekana Héritier Luvumbualionekana akifunga mdomo wake kwa mkono wake wa kushoto, huku akielekeza vidole vyake viwili kichwani, baada ya kufunga bao moja kwa bila.

Ishara hiyo hiyo inalenga kukemea ukimya wa Jamii ya Kimataifa kuhusu mauaji ambayo yamekuwa yakifanyika nchini mwake, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Serikali ya DRC inailaumu Rwanda kama nchi inayotoa msaada kwa moja ya makundi makuu ya waasi yaliyoteka maeneo ya mashariki mwa DRC, M23

Tuhuma kama hizo pia zimeungwa mkono na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, lakini Rwanda inakanusha kuhusika na mzozo huo.

    BBC

No comments