Longido, Arusha: Vijana 70 wakamatwa na chuo chao kufungwa wakifundishwa karate na mafunzo ya siasa kali

 


Kamati ya Ulinzi na usalama Wilaya ya Longido Mkoa wa Arusha imekifunga chuo kimoja cha mafunzo ya kiislam kwa kutishia Amani na usalama wa nchi ambapo wamewakuta vijana walioachishwa shule za msingi na sekondari walioenda kufunzwa Imani Kali na mapigano (Karate na judo)

Mkuu wa Wilaya ha Longido amefanya hilo leo baada ya kamati ya usalama kupata taarifa juu ya mafunzo yanayofanywa kwenye chuo hiko kisichosajiliwa.

Kimsingi vyuo hivi vipo sehemu mbalimbali nchini na ni hatari kwa usalama wa nchi kwani vijana hawa huchukuliwa sehemu mbalimbali kwa lengo la kuja kufundishwa dini na itikadi mbali.

No comments