Dunia yafika kiwago cha juu cha joto cha zaidi ya 1.5C kwa mwaka mzima

 

Kwa mara ya kwanza, ongezeko la joto duniani limezidi 1.5C katika mwaka mzima, kulingana na huduma ya hali ya hewa ya EU.

Viongozi wa dunia waliahidi mwaka wa 2015 kujaribu kupunguza ongezeko la joto la muda mrefu hadi 1.5C, ambayo inaonekana kama muhimu kusaidia kuzuia athari mbaya zaidi.

Ukiukaji huu wa mwaka wa kwanza hauvunji 'makubaliano ya Paris' ya kihistoria, lakini inaleta ulimwengu karibu na kufanya hivyo ndani ya kipindi cha muda mrefu.

Hatua za haraka za kupunguza uzalishaji wa kaboni bado zinaweza kupunguza ongezeko la joto, wanasayansi wanasema.

"Kupitia [1.5C ya ongezeko la joto] kwa wastani wa kila mwaka ni muhimu," anasema Prof Liz Bentley, mtendaji mkuu wa Jumuiya ya Kifalme ya Hali ya Hewa.

"Ni hatua nyingine katika mwelekeo mbaya. Lakini tunajua tunachopaswa kufanya."

Kupunguza ongezeko la joto la muda mrefu hadi 1.5C juu ya viwango vya "kabla ya viwanda" - kabla ya wanadamu kuanza kuchoma mafuta mengi - imekuwa ishara kuu ya juhudi za kimataifa za kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Ripoti ya kihistoria ya Umoja wa Mataifa mwaka 2018 ilisema kwamba hatari kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa - kama vile mawimbi makali ya joto, kupanda kwa kina cha bahari na kupoteza wanyamapori - ni kubwa zaidi katika 2C ya joto kuliko 1.5C.


No comments