Mwenyekiti UVCCM Mbarali azungumza na Kikwete
Mwenyekiti wa Umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi UVCCM wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya, Medson Mwambapa amemtembelea na kufanya mazungumzo na Rais mstaafu wa awamu ya Nne Mhe. Jakaya Kikwete nyumbani kwake Kawe Bahari Beach jijini Dar es salaam.
Katika mazungumzo yao wamejadili namna ya kutumia nguvu ya umoja wa vijana katika kuendelea kuimarisha chama katika Wilaya ya Mbarali, sambamba na kusaidia vijana hao kunufaika na fursa mbalimbali zilizopo ndani na nje ya Chama.
Ikiwa ni muendelezo wa dhamira chanya na mchakato wa kuwaondoa Vijana katika Wimbi la Changamoto ya Ajira.
#UvccmMbarali
#MedsonMwambapa
#WasafiDigitalUpdate

Post a Comment