Tripple C awataka Simba kuondoa tofauti

 


KIUNGO fundi kutoka Zambia, Clatous Chota Chama maarufu kama Tripple C, amewataka mashabiki wa timu yake kuondoa tofauti zao na kushikana pamoja, wakati wakienda kujiuliza dhidi ya Namungo, wakitokea kupata kipigo kibaya cha mabao 5-1 kutoka kwa mahasimu wao Yanga.

Mara baada ya mchezo huo, kumekuwa na maneno mengi, ikiwamo tuhuma kwamba kulikuwa na hujuma miongoni mwa wachgezaji, wakiwemo Chama ambao walihongwa ili kucheza chini ya kiwango. Aidha, kumekuwa na taarifa mitandaoni kuwa wachezaji kadhaa, akiwemo kiungo huyo mshambuliaji, kutokana na tuhuma za hujuma.

No comments