BILIONI MBILI ZATUMIKA KUNUNULIA MTAMBO DMI

 

  • Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya
    Uchukuzi imetumia zaidi ya shilingi bilioni mbili kununulia mtambo
    maalum wa kidigitali wa kunyakulia mizigo (Crane Simulator) ili
    kurahisisha mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wanaosoma kozi za
    uendeshaji mitambo katika wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI).
    Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Mkuu wa
    Chuo cha DMI Dkt. Tumaini Gurumo amesema elimu ya uendeshaji wa
    mitambo unahitaji wahitimu kufanya mazoezi ya nadharia na vitendo ili
    kuwezesha kuwa mahiri katika utendaji.
    “Kozi za uendeshaji wa mitambo hususani kwenye mitambo ya
    kunyakua vitu vizito zinahitaji uzoefu kwenye nadharia na vitendo hivyo
    kupitia mtambo huu wanafunzi watatakiwa kufuzu kwenye maeneo yote
    ili kuwezesha kufanya kazi kwa weledi, tunaishukuru sana Serikali ya
    awamu ya Sita kwa kuwezesha jambo hili” alisema Dkt. Tumaini.
    Dkt. Tumaini amesema Serikali imeendelea kutoa fedha kwa chuo cha
    DMI lengo likiwa kuhakikisha chuo hicho kinazalisha wataalam
    watakaoweza kushindana sokoni lakini pia kuweza kuendesha miradi
    mikubwa inayotekelezwa nchini hasa miradi ya ujenzi wa meli katika
    maziwa Nchini.
    Kwa upande wake Mkufunzi wa DMI, Elinathan Blasius amesema
    mtambo huo wa kisasa unaotumia teknolojia ya kompyuta
    utawawezesha wahitimu kwenda na wakati hasa kwenye upakiaji na
    upakuaji wa mizigo katika bandari, Viwandani na kwenye migodi.
    Kwa upande wake Mwalimu Leonard Mwesiga ametoa rai kwa
    wanafunzi wanaopenda kujiunga na kozi hiyo kutuma maombi ili
    kuongeza wataalam kwenye eneo la uendeshaji mitambo.
    (Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Uchukuzi)

No comments