LESOTHO YATAKA MIJI YA AFRIKA KUSINI KUREJEA KATIKA MIPAKA YAKE
Bunge la Lesotho linatarajiwa
siku ya Jumatano kujadili hoja kuhusu kurejeshwa kwa baadhi ya maeneo ya Afrika
Kusini chini ya himaya yake.
Mbunge wa upinzani anataka
wabunge "kutangaza eneo lote la Free State, sehemu za Rasi ya Kaskazini,
sehemu za Rasi ya Mashariki, sehemu za Mpumalanga na sehemu za KwaZulu-Natal
kama sehemu ya eneo la Lesotho", kulingana na karatasi ya agizo la bunge.
Inasema urejeshaji huo
utatekelezwa chini ya Azimio nambari 1817 la Umoja wa Mataifa (XVII) ambalo
lilipitishwa na Baraza Kuu mnamo Desemba 1962.
Kihistoria, watu wa Lesotho
walipatikana katika Orange Free State ya Afrika Kusini, Eastern Cape, Northern
Cape, Mpumalanga na sehemu za KwaZulu-Natal.
Lakini walilazimishwa kuhamia
Lesotho ya sasa kwa sababu ya vita.


Post a Comment