MWALIMU AKAMATWA KWA KUISHI KINYUMBA NA MWANAFUNZI

 millardayo Twitterren: "Mwalimu wa Shule ya Msingi Lolesha Wilayani Nkasi,  Rukwa Charles Bulinga (28) anashikiliwa na Polisi akituhumiwa kumbaka  mwanafunzi wake wa Darasa la nne, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa  amethibitisha>”Raia

MWALIMU wa Shule ya Msingi Itete kata ya Kirando Wilayani Nkasi, Clarence Mwanakurya (29) amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za kumuoa Mwanafunzi wa kidato cha kwanza Jesca Mwanji (20) tangu mwaka jana na kuishi nae katika majengo ya Serikali yaliyopo katika Shule ya Msingi Itete anaposoma Mwanafunzi huyo.

Haya yamebainika baada ya Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, Peter Lijuakali kuanza oparesheni ya kuzuia na kupambana na mimba za utotoni ambapo amewataka Walimu wa Msingi na Sekondari kuziheshimu sketi za shule kwani zitawaletea matatizo katika kazi zao na maisha kwa ujumla, oparesheni hiyo imeanza tarehe 01.11.2021 itaendelea mpaka wabainike waliowaachisha Shule Wanafunzi na kuwaoa.

Sambamba na tukio hilo, pia Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo naye amekamatwa pamoja na Clarence, sababu ya Mwalimu Mkuu kukamatwa ni kukaa kwake kimya na kuruhusu Clarence kuishi kuishi na Mwanafunzi huyo.

No comments