WAZIRI MKUU AKATAA TAASISI ZA NIDA, RITA KUUNGANISHWA
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, amesema
serikali haiwezi kuunganisha taasisi za Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa
(NIDA) na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kutokana na tofauti za
majukumu yake.
Waziri mkuu alisema hayo jana Bungeni mjini
Dodoma, akijibu swali la Abubakari Damian Asenga, mbunge wa Kilombero ambaye
alishauri taasisi hizo ziunganishwe ili kurahisisha upatikanaji wa vitambulisho
vya Taifa ambavyo alisema kwa sasa vinacheleweshwa sana.
Alisema kuwa sababu kubwa inayosababisha
kuchelewa kutolewa vitambulisho vya Taifa kwenye mikoa ya pembezoni ni
kujiridhisha kwa mtu anayeomba kama ni mtanzania au sio mtanzania.
"nataka niwahakikishie yeyote mtanzania
mwenye baba na mama mtanzania atapata kitambulisho "amesema Mhe. Kassim
Majaliwa

Post a Comment