MWENGE WA UHURU WABARIKI BILIONI 11 MTWARA, WAINGIA RUVUMA

 Single News | Arusha Regional

MWENGE wa Uhuru ambao umekuwa ukikimbizwa kila mwaka, umemaliza kazi katika Mkoa wa Mtwara ambako ulizindua jumla ya miradi 42, yenye thamani ya shilingi bilioni 11 na sasa umeingia mkoani Ruvuma.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Brigedia Jenerali Marco Gaguti amekabidhi mwenge huo kwa mwenzake wa Ruvuma Brigedia Jenerali Balozi Wilbart Mbuge katika kijiji cha Sauti moja wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma. 

Brigedia Gaguti amesema ukiwa mkoani Mtwara mwenge uliweka mawe ya 
msingi, kuzindua, kuona na kukagua jumla ya miradi 42 yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 11.

Brigedia Jenerali Gaguti amesema ukiwa mkoani humo mwenge wa uhuru umekimbizwa katika wilaya tano na kupita katika urefu wa kilometa 556.

Brigedia Jenerali Gaguti amesema miradi hiyo imetekelezwa na serikali kwa kushirikiana na nguvu za wananchi.

Amesema miradi ambayo imebainika kuwa na kasoro atakaa na watendaji wake ili kufanya marekebisho na kuhakikisha miradi hiyo inatoa huduma bora kwa wananchi.

No comments