MVUTANO MKALI WA MAWAKILI KESI YA MBOWE

MVUTANO mkali unaendelea katika Mahakama
Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumi Uchumi, jijini Dar es Salaam, baina
ya mawakili wa upande wa Jamhuri na Utetezi katika kesi ya Ugaidi inayomkabili
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na
wenzake watatu.
Kesi imesimama kwa dakika 30 kwa ajili ya mapumziko baada ya
upande wa Jamhuri kuwasilisha hoja zao kuhusu mapingamizi matatu ya upande wa
utetezi yaliyowekwa Septemba Mosi mwaka huu ambapo Mahakama hiyo itatoa uamuzi.
Mapingamizi hayo ni pamoja na hati ya mashitaka kukosa
viashiria vya makosa, kushtaki watuhumiwa kwa kosa la kula njama na makosa
mengine kinyume na utaratibu wa kuandaa hati ya mashitaka.

Post a Comment