MWANA FA APATA AJALI MOROGORO

 Mwana FA joins Tanzania's National Arts Council | Music In Africa

 

MSANII mkongwe wa Hip Hop ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Muheza kupitia chama tawala, Hamis Mwijuma maarufu kama Mwana FA, amepata ajali ya gari mkoani Morogoro leo.

 

Kamanda wa Polisi Morogoro Fortunatus Musilim amesema Mbunge huyo yupo salama.

“Nimepata hiyo taarifa, nimetuma Vijana wangu huko kupata Habari kamili, Mheshimiwa yupo salama lakini kuna wachache wamepata mshtuko na hata Gari yake ndiyo imetumika kuwapeleka baadhi yao Hospitali” ——— RPC Musilim. 

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Martine Shigela amesema walionusurika kwenye ajali hiyo ni Watu watano na walipopatia ajali ni Kingolwira Manispaa ya Morogoro.

 

No comments