NAHODHA WA SERENGETI BOYS ATUA LIGI KUU SERBIA

MOURICE Abraham, aliyekuwa nahodha wa kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana chini ya umri wa miaka 17, amejiunga na timu ya Spartak Subotika inayoshiriki Ligi Kuu nchini Serbia.
Kiungo huyo amesaini mkataba wa miaka minne na klabu hiyo akiwa chini ya usimamizi wa Samaplayer Management na tayari kijana yupo Serbia akisubiri kutambulishwa.
Kampuni hiyo inayomsimamia
inaongozwa na nahodha wa timu ya Taifa Stars, Mbwana Samatta kupitia ktk
ukurasa wake wa Instagram tayari imeweka moja ya video za mchezaji huyo akiwa
katika majukumu yake mapya nchini Serbia.
Licha ya kusajiliwa katika timu
ya wakubwa ataanzia kuchezea soka lake katika timu ya vijana chini ya miaka 19
na baadaye ataitumikia timu ya wakubwa.

Post a Comment