MAMA SAMIA, TEMBELEA PPRA KUNA MADUDU

WAFANYABIASHARA, wakitambua dhamira njema ya Rais Samia Suluhu Hassan, wamemuomba atembelee PPRA ili ajionee madudu yanayoendelea ili mradi kuwakwamisha wao kufanya majukumu yao.
Mmoja wa wafanyabiashara hao
amelaumu mfumo wa tenda za serikali (TanePs), kwamba una lengo la
kuwakwamisha, kwani leo ikiwa ni siku ya mwisho ya kuomba tenda za ICT equipments
Supply, mfumo hio tangu asubuhi hauko sawa.
Lakini pia, baadhi ya watumiaji wa
TanePs account zao za kuombea hizo tenda zimekuwa blocked kutokana na kujaribu
ku-log in mara nyingi. Bila huruma wafanyakazi wa PPRA wamekuwa na majibu ya
dharau na kutokuwa na msaada.
Leo licha ya kutokea changamoto hii, mtu wa idara ya IT hapo
PPRA ametoka ofisini makao makuu kabla ya muda na kurudi nyumbani kwake kabla
ya muda wa kazi huku akiacha mamia ya Wafanyabiashara wasijuenini cha kufanya.
"Hii nchi ina watu wanaikwamisha kwa makusudi, naiomba
serikali ifuatilie PPRA Kuna madudu mengi sana. Inakuaje kila mwaka mfumo
unakuwa unasumbua? Kama watu wameshindwa kazi mbona Kuna mamilion ya vijana
wazuri mitaani wanaweza kufanya hiyo kazi kwa ufasaha zaidi. Yaani taasisi ya
umma inaendeshwa kama genge?, amelalama mfanyabiashara huyo.
"Hatuwezi kukubali hii ni nchi yetu sote. Mama Samia tembela
hapo PPRA uwaulize kwa nini mifumo yao inasumbua kila siku na kwanini hawataki
kufungulia watu account zao zilizokuwa blocked."

Post a Comment