TFS kuuza miti aina ya Misaji kielektroniki
Wakala
wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) utauza
miti aina ya misaji yenye jumla ya
meta za ujazo 7,410.001 iliyopo
katika Shamba la miti Longuza, Muheza Mkoani Tanga na Shamba la miti Mtibwa lililopo
Turiani Mkoani Mororgoro. Jumla ya meta za ujazo 4,647.081 na 2,762.92 zitauzwa katika Shamba la miti Longuza
na Mtibwa mtawalia.
1.
Miti ya Misaji itauzwa kwa njia ya
mnada wa kielektroniki kwa kuzingatia Kanuni ya 31 (ii) ya Kanuni za Misitu za Mwaka 2004. Mnada huu utafanyika siku ya Alhamisi tarehe
14 Machi, 2024
kuanzia saa mbili kamili (02:00)
asubuhi hadi saa sita na dakika thelethini na mbili (06:32) mchana kwa Shamba
la miti Longuza
na Ijumaa tarehe 15 Machi, 2024 kuanzia saa mbili kamili (02:00)
asubuhi hadi saa nne na dakika kumi na tano (04:15) asubuhi kwa Shamba la miti Mtibwa.
1.
Ili kushiriki kwenye mnada, mshiriki atatakiwa
kujisajili kupitia anuani ifuatayo
http://mis.tfs.go.tz/e-auction kuanzia tarehe ya tangazo hili hadi
saa tisa kamili (9:00) mchana siku ya
tarehe 12 Machi 2024 siku ya Jumanne. Kwa ajili ya msaada wa usajili, wasiliana na:
+255 713 335 926 or +255 766 857 062.
2.
Washiriki wanakaribishwa kukagua
miti iliyopo shambani wakati wa saa za kazi;
kuanzia saa tatu (3:00) asubuhi hadi saa tisa (9:00) alasiri siku za Jumatatu hadi Ijumaa isipokuwa siku za
sikukuu. Ukaguzi huo utafanyika kuanzia
tarehe ya Tangazo hili hadi tarehe 13 Machi 2024 siku
ya Jumatano.
Wahifadhi wakuu wa Mashamba husika au wasaidizi wao watakuwepo kwa ajili ya
kutoa maelezo ya ziada.
Masharti ya kushiriki Mnada huu
1. Mshiriki anapaswa kujisajili na kuthibitisha ushiriki wake kupitia http://mis.tfs.go.tz/e-auction;
Muhimu:
Uthibitisho baada ya mnada kuanza hautakubaliwa.
1.
Malipo yote yafanyike kupitia
benki au mitandao
ya watoa huduma za kifedha baada ya kupokea hati ya madai
(bill) ya Mfumo wa Makusanyo ya Serikali
(GePG) itakayopatikana kwenye akaunti
ya mshiriki kwenye mfumo wa mnada wa kielektroniki,
2.
Mshiriki atakayeshinda atatakiwa
kulipa asilimia ishirini na tano (25 %) ya thamani yote ya ununuzi ndani ya siku tatu (3) za
kazi baada ya siku ya mnada. Fedha
hizo hazitarudishwa endapo mshindi atashindwa kulipia ujazo aliouziwa. Mnunuzi ataruhusiwa kulipia zaidi ya asilimia 25 ya malipo
ya kitalu chochote mara tu baada ya kukamilisha
malipo ya awali ya 25% kwa vitalu vyote
alivyonunua. Asilimia sabini na tano (75 %) iliyobaki italipwa ndani ya siku kumi na nne (14) kuanzia siku ya
mnada,
3.
Mshiriki atakayefanikiwa kununua miti ya misaji hataruhusiwa kusafirisha magogo nje ya nchi
kwa mujibu wa kanuni ya 50 (1) ya kanuni za misitu za mwaka 2004,
1.
Mshiriki aliyeshinda mnada
atatakiwa kuondoa mazao ya misitu aliyonunua
ndani ya miezi miwili (siku sitini) baada ya
kumaliza kulipa malipo yote kwa asilimia
100. Aidha, endapo kutajitokeza changamoto ambazo zitasababisha kushindwa kuondoa mazao hayo ya misitu kwa muda uliopangwa, barua rasmi iwasilishwe kumjulisha Mhifadhi Mkuu wa Shamba kwa maamuzi,
2.
Miti hiyo ya misaji itauzwa mahali
ilipo na jinsi ilivyo na mnunuzi hatakuwa na
haki ya kudai
fidia baada ya mauzo kufanyika.
Wajibu wa Wakala wa Huduma za Misitu
Tanzania;
1.
Kupanga ploti za kuuza kama zinavyooneshwa katika Jedwali la orodha ya bei za kianzio (mrabaha
tu) kwa mita moja ya ujazo, na
2.
Kutoa barua za ushindi na hati za madai kwa wanunuzi walioshinda mnada kwa kila ploti mara baada ya kumalizika kwa mnada.
Ploti za Miti ya Misaji inayouzwa
Ploti
zimepangwa kwa mafungu, ambapo kila baada ya masaa mawili na robo(2:15) fungu moja litauzwa. Vilevile ndani ya muda wa mnada uliotengwa kutakuwa
na mapumziko (waterbreak) ya dakika mbili
kila baada ya fungu moja kuuzwa.
Ploti
zinazouzwa zimeorodheshwa katika jedwali namba
1 na jedwali namba 2 kama ifuatavyo: -
JEDWALI Na. 1; ORODHA YA PLOTI ZITAKAZOUZWA KATIKA
SHAMBA LA MITI
LONGUZA SIKU YA ALHAMISI
TAREHE 14 MACHI, 2024
|
NA. |
JINA LA KIUNGA |
UJAZO KWA KILA KIUNGA
(M3) |
BEI
PENDEKEZWA (TZS) |
FUNGU LITAKALO UZWA |
|
1 |
KH1-t25 |
79.719 |
500,000.00 |
Fungu Na. 1 |
|
2 |
KH1-C2 |
72.711 |
693,000.00 |
|
|
3 |
KH1-C3 |
56.484 |
693,000.00 |
|
|
4 |
KH1-C4 |
65.239 |
693,000.00 |
|
|
5 |
KH4-A11 |
86.756 |
780,000.00 |
|
6 |
KH4-A13 |
160.792 |
780,000.00 |
|
|
7 |
KH4-A14 |
100.271 |
780,000.00 |
|
|
8 |
KH4-A15 |
127.224 |
780,000.00 |
|
|
9 |
KH4-A16 |
120.269 |
780,000.00 |
|
|
10 |
KH4-A17 |
185.444 |
780,000.00 |
|
|
11 |
KH4-28 |
109.527 |
780,000.00 |
|
|
12 |
KH4-29 |
165.361 |
780,000.00 |
|
|
13 |
KH4-30 |
145.365 |
780,000.00 |
|
|
14 |
KH4-31 |
161.347 |
780,000.00 |
|
|
15 |
KH4-32 |
75.336 |
780,000.00 |
|
|
16 |
KH4-33 |
151.944 |
780,000.00 |
|
|
17 |
KH4-34 |
121.58 |
780,000.00 |
|
|
18 |
KH4-35 |
47.132 |
780,000.00 |
|
|
19 |
KH4-36 |
71.805 |
780,000.00 |
|
|
20 |
KH4-37 |
137.014 |
780,000.00 |
|
|
21 |
KH4-38 |
81.665 |
780,000.00 |
Fungu Na. 2 |
|
22 |
KH4-39 |
165.478 |
780,000.00 |
|
|
23 |
KH4-40 |
112.172 |
780,000.00 |
|
|
24 |
KH4-41 |
111.185 |
780,000.00 |
|
|
25 |
KH4-42 |
155.527 |
780,000.00 |
|
|
26 |
KH4-43 |
120.523 |
780,000.00 |
|
|
27 |
KH4-44 |
116.884 |
780,000.00 |
|
|
28 |
KH4-45 |
47.794 |
780,000.00 |
|
|
29 |
KH4-46 |
49.717 |
780,000.00 |
|
|
30 |
KH4-47 |
131.877 |
780,000.00 |
|
|
31 |
KH4-48 |
153.638 |
780,000.00 |
|
|
32 |
KH4-49 |
103.264 |
780,000.00 |
|
|
33 |
KH4-50 |
67.077 |
780,000.00 |
|
|
34 |
KH4-51 |
64.208 |
780,000.00 |
|
|
35 |
KH4-52 |
161.421 |
780,000.00 |
|
|
36 |
KH4-53 |
95.21 |
780,000.00 |
|
|
37 |
KH4-54 |
45.142 |
780,000.00 |
|
|
38 |
KH4-55 |
185.177 |
780,000.00 |
|
|
39 |
KH4-56 |
120.343 |
780,000.00 |
|
|
40 |
KH4-57 |
166.063 |
780,000.00 |
|
|
41 |
KH4-58 |
151.396 |
780,000.00 |
|
|
|
JUMLA KUU |
4647.081 |
|
|
JEDWALI Na. 2: ORODHA YA PLOTI
ZITAKAZOUZWA KATIKA SHAMBA LA MITI
MTIBWA SIKU YA IJUMAA TAREHE 15 MACHI, 2024
|
Na. |
JINA LA KIUNGA |
UJAZO (M3) |
BEI PENDEKEZWA (Tshs/Cbm) |
FUNGU LITAKALO UZWA |
|
1 |
LR16A-30 |
472.621 |
365,000 |
Masaa 2 na dakika 15 |
|
2 |
LR 16 A-33 |
462.151 |
300,000 |
|
|
3 |
LR 16 A-35 |
442.266 |
300,000 |
|
|
4 |
LR 16 A-37 |
255.487 |
180,000 |
|
|
5 |
LR 16 A-38 |
260.584 |
250,000 |
|
|
6 |
LR 16 A-39 |
467.758 |
250,000 |
|
|
7 |
LR18-9 |
232.641 |
600,000 |
|
|
8 |
LR18-11 |
169.416 |
600,000 |
|
|
JUMLA |
2,762.92 |
|
|
|
Tangazo hili linapatikana katika tovuti zifuatazo za: www.tfs.go.tz na www.mnrt.go.tz

Post a Comment