NMB, CTM TANZANIA WAZINDUA MIKOPO YA KUMALIZIA UJENZI

 


BENKI ya NMB wamesaini makubaliano na Kampuni ya CTM Tanzania yaliyopewa jina la ‘Lipa Baadae,’ yatakayowawezesha wateja wa benki hiyo kupata mikopo ya fedha za manunuzi ya bidhaa za umaliziaji ujenzi wa nyumba ‘finishing,’ zinazouzwa na kampuni hiyo, huku wakinufaika na punguzo la asilimia 2 hadi 10.

Lipa Baadae ni mfumo utakaowawezesha wateja wa NMB na CTM kupata suluhu za kifedha kupitia mikopo ya kuboresha nyumba, kununulia bidhaa za kampuni hiyo bobevu kwa usambazaji na uuzaji wa marumaru ‘tiles’, vyoo, majakuzi, mabeseni ya kunawia na kabati za bafuni na vyooni, pamoja na ushauri wa vipimo vya ujenzi bure.

Hafla ya kusaini makubaliano hayo imefanyika Jumatano Novemba 21, katika Ofisi za CTM Tanzania zilizoko Barabara ya Mwai Kibaki, Kawe jijini Dar es Salaam, ambako NMB iliwakilishwa na Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi na Biashara, Filbert Mponzi huku CTM ikiwakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wake Shiraz Satchu.

No comments