STAA AREKODIWA AKIFANYA MAPENZI, AKATAA KUTOA FEDHA ILI USIVUJISHWE
STAA wa Muziki Kutokea Nchini
Nigeria Tiwa Savage amefunguka kutumiwa mkanda wa Ngono (Sex Tape)
Akiwa Kwenye Interview na The Angel Martin
Show (POWER 105.1) Nchini Marekani amesema kwamba
mkanda huo unaonesha ni wa kwake pamoja na mtu ambaye yupo kimahusiano naye kwa
sasa
"Jana nilikiwa njiani kwenye gari langu meneja wangu
akanitumia ujumbe kwamba kuna video amenitumia niitazame. Nilishtuka na kushangaa
pindi nilipoiona na kujiuliza kaipata wapi.
Ilikuwa ni kama baada ya dakika 20
kufanyika, huo mkanda alitumiwa kijana wetu mmoja kwenye timu yetu ikituonyesha
mimi na mtu ambaye niko naye kwenye uhusiano.
Nilichanganyikiwa na kumuuliza meneja tunafanyaje, meneja
wangu akaniuliza ni kiasi gani anahitaji tumpatie? Nikamwambia hapana kwa
sababu tukimpa leo, atarudi tena baada ya miezi miwili mbelen atahitaji tena,
siwezi ruhusu mtu kuniibia kwa kitu ambacho si halali."

Post a Comment