WACHEZAJI WOTE WAZAWA KUBAKI SIMBA -GOMES


Inaweza kuwa picha ya mtu mmoja au zaidi, watu wanasimama, watu wanacheza spoti na nyasi

KOCHA Mkuu wa Klabu ya Simba Didie Gomes da Rosa amesema anatamani wachezaji wote wazawa wa timu hiyo wabakie kikosini msimu ujao.

"Toka nimejiunga na Simba nimegundua kwamba wachezaji nilionao ni bora kuliko waliopo timu zingine hapa Tanzania ni kipaumbele changu kuwabakisha klabuni hapa.

Sitoruhusu mchezaji wa kitanzania yoyote aondoke Simba ila kama anataka kuondoka au hafanyi ninavyotaka milango iko wazi kuondoka." alisema Gomes na kusisitiza haoni kama kuna mchezaji yoyote Tanzania ana kitu cha ziada kuwazidi wachezaji alionao pale msimbazi.

Wachezaji wa simba wanaomaliza mikataba yao mwishoni mwa msimu huu..

1.Ibrahim Ajibu

2.Francis Kahata

3.Miraji Athumani

4.Ally Salim

5.Beno Kakolanya

6.Gadiel Michael

Kwa upande wa Kocha wa makipa Milton Nienov amesema kwake yeye makipa wote watatu(Salim, Kakolanya na Manula) wabaki kikosini msimu ujao.

Gomes amesema pia bado kuna mechi kadhaa za kucheza kwahiyo mchezaji asipocheza mechi hii anaweza kucheza inayofuata.

 

No comments