Mzozo kati ya Iran na Pakistan: Hali ni tete
Pakistan imeanzisha mshambulizi ya kulipiza kisasi nchini Iran mapema siku ya Alhamisi, siku mbili baada ya Iran kushambulia ardhi ya Pakistan.
Waziri wa masuala ya kigeni nchini Pakistan alisema kwamba baadhi ya watu waliuawa katika eneo la Sistan mkoani Balushistan.
Watu tisa waliuawa kufuatia shambulio hilo kulinga na vyombo vya Habari vya Iran
Pakistan ilisema mashambulizi yake yamepiga "maficho ya magaidi" katika mkoa wa Sistan-Baluchestan nchini Iran
Pakistan ilisema ilichukua hatua kwa kuzingatia "intelijensia ya kuaminika ya shughuli kubwa za kigaidi zinazoendelea" na kusema kwamba "magaidi" kadhaa waliuawa.
Imeongeza kuwa "inaheshimu kikamilifu" mamlaka na uadilifu wa ardhi ya Iran lakini hatua yake ya Alhamisi ilikuwa "dhihirisho la azimio lisiloyumba la Pakistan la kulinda usalama wa taifa lake dhidi ya vitisho vyovyote."
Pakistan ililaani vikali shambulio la Iran siku ya Jumanne, ambalo lilipiga eneo la jimbo la Balochistan nchini Pakistan karibu na mpaka wa Iran.
Iran ilisisitiza kuwa mashambulizi yake yalilenga tu Jaish al-Adl, kundi la Waislamu wa kabila la Baloch Sunni ambalo limefanya mashambulizi ndani ya Iran, na sio raia wa Pakistan.

Post a Comment