Korea Kusini yafanya majaribio ya silaha chini ya maji
Korea Kaskazini inasema imefanyia majaribio "mfumo wa silaha za nyuklia chini ya maji" kujibu mazoezi ya pamoja ya kijeshi ya Marekani, Korea Kusini na Japan, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya serikali.
Jaribio la ndege ya "Haeil-5-23", jina ambalo Korea Kaskazini imezipa ndege zake zisizo na rubani zenye uwezo wa nyuklia chini ya maji, lilifanyika katika maji ya pwani yake ya mashariki.
Korea Kaskazini imefanya majaribio kama hayo hapo awali.
Lakini la hivi punde linakuja huku kukiwa na ongezeko kubwa la matamshi makali yabserikali ya Kaskazini.
Imesema mara kwa mara kwamba inaunda safu yake ya kijeshi katika kujiandaa kwa vita ambavyo vinaweza "kuzuka wakati wowote" kwenye peninsula.
Kiongozi wake Kim Jong Un wiki hii alitangaza kuwa lengo la kuungana upya limekamilika na kutaja Korea Kusini kama "adui mkuu".
Kauli zake pia zimefuatia hatua kadhaa zinazodaiwa katika uwezo wa kijeshi na nyuklia wa nchi yake - ikiwa ni pamoja na katika operesheni zake za chini ya maji.
Septemba iliyopita, Korea Kaskazini ilifichua kile ilichodai kuwa ni manowari yake ya kwanza yenye uwezo wa kurusha silaha za nyuklia.
Tangu Machi 2023, pia imedai majaribio ya mfumo wake wa Haeil - ndege zisizo na rubani zenye silaha za nyuklia zisizo na rubani chini ya maji.
Machache yanajulikana kuhusu silaha hizi au utendaji wao unaodaiwa lakini wachambuzi wanasema ni silaha muhimu kidogo kuliko makombora ya balistiki ya nyuklia ya Korea Kaskazini.

Post a Comment