MRUSI ATIMULIWA INDONESIA KWA KUKAA UCHI MLIMA MTAKATIFU


Mwanaume mmoja raia wa Russia ametimuliwa nchini Indonesia baada ya kubainika kuvua nguo zake na kubaki uchi wa mnyama katika Mlima Agung ambao unaabudiwa kama Mlima Mtakatifu.

Mwanamume huyo aliyetambulika kwa jina moja la Yuri, ameomba msamaha lakini atazuiwa kuingia tena Indonesia kwa angalau miezi sita.

Indonesia ambayo Mji wake mkuu ni Bali, hivi karibuni imeongeza juhudi za kukabiliana na watalii wa kigeni wanaotajwa kukosa maadili.

Mlima Agung, sehemu ya juu zaidi katika kisiwa hicho, inaaminika na Wahindu kuwa makao ya miungu. Afisa wa eneo alisema ‘hakuna kisingizio’ kwa tabia yake.

"Alikiuka kanuni na hakuonyesha heshima kwa utamaduni wetu," Mkuu wa Ofisi ya Sheria na Haki za Kibinadamu ya Bali, Anggiat Napitupulu aliambia Jakarta Post.

Katika video iliyowekwa kwenye Instagram kwa lugha ya Kirusi, Yuri alisema: "Kitendo changu hakina kisingizio. Kitu pekee kilichosababisha kilichotokea ni ujinga wangu binafsi."

Baadaye alishiriki katika hafla maalum ya utakaso wa mlima huo - tambiko ambalo mara nyingi hufanyika na wenyeji baada ya matukio kama haya.

Wijaya, balozi mdogo wa heshima wa Urusi huko Bali, aliiambia CNN Indonesia kwamba mtalii huyo alikuwa ‘mwehu’ na kwamba kumfukuza ni jambo sahihi kufanya. Wenyeji wengi kwenye mitandao ya kijamii pia waliunga mkono kufukuzwa kwake.

 

 

No comments